EL CLASICO NI VITA KATI YA
Messi Vs Ronaldo
Neymar Vs Bale
>>LEO JUMAMOSI
OKTOBA 26, NOU CAMP, SAA 1 USIKU
NI EL CLASICO ya 167 ndani ya Nou Camp
Jijini Barcelona wakati FC Barcelona na Real Madrid zitakapocheza Mechi ya
La Liga huku macho ya Washabiki safari hii yakiwakodolea ‘Wapya’ Gareth Bale na
Neymar pamoja na kuwakazia wale wale wa zamani Cristiano Ronaldo na Lionel
Messi.
Ni Mechi pia itakayowakutanisha
Mameneja wapya kwa Timu zote, Carlo Ancelotti toka Italy kwa Real Madrid na
Gerardo Martino toka Argentina kwa Barcelona.
Wikiendi iliyopita, Barcelona
walipoteza Pointi zao za kwanza kwenye La Liga baada ya kutoka Sare 0-0 na
Osasuna na Real Madrid kushinda na kuwakaribia Barcelona ambao wako kileleni
Pointi 3 mbele yao.
Mvuto kwa El Clasico hii ni Klabu zote
mbili kuwa na Wachezaji wapya ambao wanaweza kucheza kwa mara ya kwanza kwenye
mtanange wa aina hii kwa Barcelona kumchezesha Mchezaji mpya Neymar waliemnunua
Msimu huu kutoka Santos ya Brazil na Real kumtumia Gareth Bale alievunja Dau la
kununuliwa kwa Bei Ghali Duniani walipomnunua kwa Euro Milioni 100 kutoka
Tottenham.
Lakini wakati Neymar akionyesha cheche
zake kwenye Timu ya Barcelona, Bale amekuwa akikumbwa na Majeruhi yaliyomfanya acheze
Mechi chache tu.
Kocha wa Real, Carlo Ancelotti, amedokeza
kuwa Bale ataanza Mechi hii pamoja na Wachezaji wake wapya wengine Isco na
Asier Illarramendi huku Cristiano Ronaldo akiongoa majeshi.
Nae, Gerardo Martino, amedokeza kuwa
mashambulizi ya Kikosi chake yataongozwa na Lionel Messi na Neymar huku ukiwepo
uwezekano wa Beki wao Mkongwe ambae pia ni Nahodha wao, Carles Puyol, kuanza
Mechi hii baada ya kurudi tena dimbani akiwa nje akijiuguza Goti lake tangu
Mwezi Machi.
+++++++++++++++++++++++
REKODI:
Uso kwa Uso:
-Real Madrid Wameshinda Mechi 90
-Barcelona Wameshinda Mechi 86
Mataji:
-Barcelona Vikombe 81
-Real Madrid Vikombe 76
+++++++++++++++++++++++
MECHI ZA MWISHO:
02-03-2013 Real Madrid: 2 FC Barcelona:
1 [La Liga]
26-02-2013 FC Barcelona: 1 Real Madrid:
3 [Copa Del Rey]
30-01-2013 Real Madrid: 1 FC Barcelona:
1 [Copa Del Rey]
07-10-2012 FC Barcelona: 2 Real Madrid:
2 [La Liga]
29-08-2012 Real Madrid 2 FC
Barcelona 1 [Super Cup]
23-08-2012 FC Barcelona 3 Real Madrid 2
[Super Cup]
MSIMAMO-Timu za Juu:
|
NA
|
TIMU
|
P
|
W
|
D
|
L
|
F
|
A
|
GD
|
PTS
|
|
1
|
FC Barcelona
|
9
|
8
|
1
|
0
|
28
|
6
|
22
|
25
|
|
2
|
Atletico de Madrid
|
9
|
8
|
0
|
1
|
21
|
7
|
14
|
24
|
|
3
|
Real Madrid CF
|
9
|
7
|
1
|
1
|
19
|
9
|
10
|
22
|
|
4
|
Villarreal CF
|
9
|
5
|
2
|
2
|
15
|
9
|
6
|
17
|
|
5
|
Getafe CF
|
9
|
5
|
1
|
3
|
14
|
11
|
3
|
16
|
|
6
|
Athletic de Bilbao
|
9
|
5
|
1
|
3
|
15
|
13
|
2
|
16
|
|
7
|
RCD Espanyol
|
9
|
4
|
2
|
3
|
12
|
11
|
1
|
14
|
+++++++++++++++++++++++
LA LIGA-WAFUNGAJI
BORA:
1 Diego Costa [Atletico Madrid] 10
1 Lionel Messi [Barcelona] 8
3 Cristiano Ronaldo [Real Madrid] 8
4 Pedro [Barcelona] 5
+++++++++++++++++++++++

No comments:
Post a Comment