Simba imetolewa hatua ya 64
Bora, sawa na raundi ya Pili tu ya Kombe la Azam Sports Federation Cup (ASFC) usiku
wa hapo jana baada KIUNGO Jonas Gerald Mkude kugongesha mwamba penalti na Mohammed
Hussein ‘Tshabalala’ akamdakisha kipa zamani wa kimataifa nchini, Shaaban
Dihile.
Maana yake, Simba SC imevuliwa ubingwa wa Azam Sports Federation baada
ya kufungwa kwa penalti 4-3 kufuatia sare ya 1-1 ndani ya dakika 90 na timu ya
Green Worriors ya Mwenge, inayomilikiwa na Jeshi la Wananchi Tanzania (JWTZ).
Katika mchezo huo uliofanyika Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, Dar es
Salaam kipa wa Simba, Aishi Manula alipangua penalti moja ya Zuakuu Mgala
kabla ya George Ossey kupiga nje, lakini penalti za Cecil Efram, Amir Hajji,
Juma Mdingi na Idd Nyambi zilimpita.
Katika dakika 90 za mchezo
huo, Green Warriors walitangulia kupata dakika ya 43 kupitia kwa mshambuliaji
Hussein Bunu aliyefunga kwa kichwa akimalizia kazi nzuri ya Gido Chawala.
Bao hilo lilidumu na hadi
kipindi cha pili, ambako Simba walifanikiwa kusawazisha dakika ya 53 kwa
penalti ya kiufundi ya Nahodha John Raphael Bocco ‘Adebayor’ baada ya Amiri
Haji kuunawa mpira kwenye boksi katika harakati za kuokoa.
Kutoka hapo, Simba walifunguka zaidi na kuanza kupeleka mashambulizi mfululizo langoni mwa Green Warriors, lakini sifa zimuendee kipa wa kikosi cha Taifa Stars kilichoshiriki CHAN mwaka 2009 nchini Ivory Coast, Shaaban Dihile aliyewaokoa michomo mingi ya hatari.
Mwishoni mwa mchezo, refa
mkongwe, Israel Nkongo alimuonyesha kadi ya njano Adam Said wa Green Warriors
na kumtoa kwa kadi nyekundu.
Makocha wote wa Simba,
Mcameroon Joseph Marius Omog na Msaidizi wake, Mrundi Masudi Juma na mzalendo,
Muharammi Mohammed ‘Shilton’ ambaye ni kocha wa makipa walijadiliana vizuri
wakati wa kuchagua wapiga penalti.
Kocha wa Green Warriors,
Azishi Kondo alikuwa mwenye furaha baada ya mechi kwa kuwatoa siyo tu mabingwa,
bali pia timu yenye makocha wawili wa kigeni na wachezaji nyota na ghali.
Lakini pamoja na Aishi
kuokoa penalti moja na Green Warriors kukosa moja, lakini haikusaidia Simba
kusonga mbele na inatolewa mapema zaidi, tena na timu ya Daraja la Pili.
Kikosi cha Green Worriors kilikuwa;
1. Shaaban Dihile,
2. Edward William,
3. Amir Hajji,
4. Cecil Efram,
5. George Ossey,
6. Iddi Nyambi,
7. Gido Chawala/Thomas Ndimbo
dk63,
8. Adam Said,
9. Mohammed Athumani,
10.
Hussein
Bunu
11.
Hassan
Gumbo/Juma Mdingi dk63.
Simba SC;
1. Aishi Manula,
2. Erasto Nyoni,
3. Ally Shomari/Mohammed
Hussein ‘Tshabalala’ dk67,
4. Yusuph Mlipili,
5. Juuko Murshid,
6. Jonas Mkude,
7. Shiza Kichuya,
8. Muzamil Yassin,
9. John Bocco,
10.
Said
Ndemla
11.
Mwinyi
Kazimoto/Moses Kitandu dk50.
No comments:
Post a Comment