HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 31 December 2017

BAADA YA TRA KUDAI KUHOJI UTAJIRI WA KAKOBE, MWENYEWE ATOKA KAULI KUHUSU UTAJIRI WAKE.



 
Ikiwa yamebaki Masaa machache kabla ya mwaka 2017 kumalizika na kuukaribisha mwaka mpya wa 2018, Askofu Mkuu wa Makanisa ya Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe ameunguruma katika ibada aliyoiongoza Leo kanisani huku akijinasibu kuwa ni Tajiri kuliko Serikali zote duniani

 Askofu wa Kanisa la Full Gospel Bible Fellowship, Zacharia Kakobe amesema kwamba yeye sio tu Tajiri kuliko Serikali ya Tanzania, Bali ni Tajiri kuliko Serikali zote duniani ikiwemo ya Marekani na Uingereza'.

" Wanaosema Kakobe amekimbia nchi nawashangaa sana sipo na wala siendi popote, kipindi Fulani walikuja kuchunguza uraia wangu lakini wakaambulia patupu, tutabanana hapa hapa" Askofu Kakobe

" Watu wanasema Niko kimya sana wala sipo kimya tatizo wanataka nizungumze wanayoyataka wao, sasa Mimi sio mtu wa namna hiyo, ukiniona nimesimama katika madhabau Hays basi ujue nina kibali cha Mungu, mtu ukitwa Mbwa kwani wewe ndio itakua Mbwa? Sasa nashangaa unaogopa nini kuitwa Mbwa wakati wewe sio Mbwa" Askofu Kakobe

No comments:

Post a Comment