HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 22 April 2014

KUBWA KULIKO MAN UNITED: GIGGS ATEULIWA MENEJA BAADA MOYES KUTIMULIWA!!



RYAN GIGGS ameteuliwa kuwa Meneja wa Muda mpya wa Manchester United baada David Moyes kutimuliwa hii Leo.
Moyes, ambae alishika wadhifa Julai Mosi Mwaka Jana, amefukuzwa kazi kufuatia Msimu mbovu wa Mabingwa hao wa England ambao wameshindwa kutetea Taji lao na pia kushindwa kufuzu kucheza UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu ujao kwa vile watakuwa nje ya 4 Bora na hii ni mara ya kwanza tangu Mwaka 1991 kwa Man United kushindwa kumaliza ndani ya 3 Bora.

Ryan Giggs, mwenye Miaka 40, ni Kocha-Mchezaji wa Man United Klabu ambayo alianza nayo tangu yuko mdogo.
Mechi ya kwanza chini ya Giggs itakuwa ni Jumamosi Aprili 26 Uwanjani Old Trafford wakati Man United itakapocheza na Norwich City kwenye Mechi ya Ligi Kuu England.
Uteuzi wa Giggs kama Meneja umepokewa vizuri na Wachezaji wa zamani wa Man United kina Dwight Yorke na David May.

Wakati May alisema Giggs ni chaguo zuri sana kwa Man United kulifanya, Dwight Yorke alisema yeye angemchagua Giggs tangu mwanzo alipostaafu Sir Alex Ferguson.
Yorke amesema: “Yeye amekuwepo Klabuni kwa Miaka 20, ni Mwekundu wa kweli na sasa anasomea Beji za Ukocha wa Kulipwa.”

Nae Mchambuzi wa Sky Sport, Jamie Carragher, amesema Giggs atafaa kwa kazi hiyo ingawa wanahitaji Kocha mzoefu kama vile Jurgen Klopp wa Borussia Dortmund.

No comments:

Post a Comment