HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 17 March 2014

TFF YALALALAMIKIWA MKOANI TANGA.


Rais wa Shirisho la soka nchini (TFF)Jamali Malinzi (kushoto)alipotembelea Ofisi za Shirikisho la Soka Africa (CAF) kulia ni Rais Mstaafu wa (TFF) Leodigar Tenga na Issa Hayatou (Katikati)


BAADHI ya Wakazi waliokuwa wamejenga katika eneo ambalo shirikisho la soka nchini kwa kushirikiana na shirikisho la soka duniani (FIFA) wanatarajiwa kujenga uwanja wa Kimataifa wamelalamika kuwa serikali bado haijawalipa fidia ili kuweza kupisha ujenzi wa uwanja huo.

Hatua ya wakazi hao inatokana na kuona Rais wa Shirisho la soka nchini (TFF)Jamali Malinzi akitembelea uwanja huo na kuanza mikakati ya ujenzi wa uwanja huo ambao unatarajiwa kugharimu mabilioni ya fedha za kitanzania.
Wakizungumza katika nyumba zao wanazoishi ndani ya eneo la shirikisho hilo lililopo Mnyanjani jijini Tanga baadhi ya waathirika hao ambao wengi wao ni akina mama Christina Lucas alisema wamekuwa wakihangaikia fidia kila kukicha kwenye ofisi ya mkuu wa wilaya ili waweze kupisha ujenzi wa uwanja wa kimataifa bila mafanikio yoyote.

Alieleza zaidi kuwa baadhi yao wameshapewa maeneo ya kwenda kujenga nyumba baada ya serikali skuridhia ombi lao lakini fidia ndio imeshindwa kutoka hadi wakati huu kitendo ambacho kinawaweka kwenye wakati mgumu.
Naye Zabila Iddy alisema wanaiomba serikali kuharakisha zoezi hilo ili shirikisho la soka la kimataifa Fifa kwa kushirikiana na CAF na TFF waweze kuanza ujenzi wa uwanja huo haraka iwezekanavyo.

Hata hivyo akizungumzia suala hilo,Mjumbe wa kamati ya utendaji
TFF,Khalid Mohamed alisema tayari taratibu za kuwalipa zilishafanyika kwa waathirika hivyo watawasiliana na viongozi wa serikali ili kujua zoezi hilo limefikia wapi. 

Jitihada za kumpata mkuu wa wilaya ya Tanga ili kuweza kuelezea
malalamiko hayo ya waathirika ambao wamedai wamekuwa wakifika kwake mara kwa mara bila mafanikio zinaendelea.

No comments:

Post a Comment