HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 17 December 2013

KIGOGO WA CCM ALIYE UWAWA KWA KUPIGWA MAWE KUZIKWA ALHAMISI


Marehemu Clement Mabina




MAZISHI ya aliyekuwa mwenyekiti wa CCM na Diwani wa Kata ya Kisesa wilayani Magu Clement Mabina, aliyeuawa kikatili na kundi la wananchi, yanatarajiwa kufanyika Alhamisi.

Taarifa iliyotolewa na msemaji wa familia ya marehemu Mabina, Timothy Gregory ambaye ni mdogo wa marehemu, alisema kwamba, mipango ya mazishi imekamilika na zaidi ni pamoja na kusubilia mtoto wa kike wa marehemu aliyoko njiani kutokea nchini Uingereza marehemu waliokuwa nje ya nchi.

Gregory alisema, Kijana mdogo wa marehemu (mtoto ) tayari amewasili jana jioni, hivyo mazishi marehemu Mabina yatafanyika kesho kutwa Kisesa wilayani Magu baada ya mtoto wake mkubwa wa kike kuwasili kutoka Uingereza.

Mwenyekiti wa Kamati ya mazishi hayo, Henry Matata ambaye ni Meya wa Manispaa ya Ilemela, amesema kuwa, taratibu za maziko ya marehemu Mabina, zinaendelea kufanyika nyumbani kwa marehemu na kupokea wageni mbalimbali wakiwemo wafanyabiashara, wanasiasa wa Kada mbalimbali kutoka vyama vya siasa na serikali pamoja na ndugu na rafiki wa karibu na marehemu wa sehemu tofauti nchini kote na nje ya nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.
Marehemu Clement Mabina (Kushoto)akiwa na Rais Jakaya Kikwete(katikati)
“Marehemu Mabina atazikwa rasmi Alhamisi saa 7:00 mchana katika shamba lake kulekule Kitongoji cha Kanyama alikouawa. Tayari tumerudisha mabango ya kuzuia watu waliokuwa wakichimba mawe na mchanga kwenye eneo hilo, yaliyoondolewa na kundi la watu waliomshambulia na majirani wamepokea na kudai eneo hilo lilikuwa likimilikiwa na marehemu kihalali kwani serikali ya kijiji ililikabidhi kwa marehemu kupitia mkutano wa hadhara hali iliyodaiwa kumuua ilikuwa kumuonea na ilitawaliwa na siasa zaidi kuliko uhalisia wa madai ya kundi la watu hao wachache .” alidai Matata.

Hadi sasa, mamia ya waombolezaji wakiwemo ndugu, jamaa, wananchi wa Kisesa, wana CCM na viongozi mbalimbali wa Chama na serikali walikuwa wakiendelea kumiminika nyumbani hapo kuomboleza.

Nacho Chama Cha Mapinduzi (CCM) mkoani Mwanza, Mwenyekiti wa CCM wa mkoa wa Mwanza, Anthony Diallo  kimetoa pole kwa wananchi wa Kisesa wakiwemo ndugu na jamaa wa familia za marehemu Mabina na mtoto Temeli Malimi (12) aliyeuawa  kwa kupigwa risasi na marehemu huyo wakati wa purukushani za kujiokoa.

Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Magu, Desidery Kiswaga alisema kwamba, marehemu Mabina aliyekuwa Mweneykiti wa zamani wa CCM mkoa wa Mwanza, atazikwa kwa heshima zote stahili.
Hivi ndivyo alivyo uwawa


No comments:

Post a Comment