HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 14 November 2013

MH DIWANI TANGA ATAKA SOKO LA SAMAKI DEEP SEA JIJINI TANGA LIFUNGWE



DIWANI wa Viti Maalumu Kata ya Chumbageni jijini Tanga kupitia chama  cha Mapinduzi (CCM)Saida Gadafi amelishauri baraza la madiwani kuridhia soko la kuuzia samaki la deepsea livunjwe kuliko kila mwaka litengewe sh.milioni 50 kwa ajili ya ukarabati wake.

Samaki wakiandaliwa kwa ajili ya kuuzwa

Gadafi alitoa kauli hiyo  wakati wa kikao cha baraza la madiwani kilichofanyika katika ukumbi wa mipango miji jijini Tanga ambapo alisema fedha hizo zinazotengwa hazionekani zinafanyia kazi gani kwa sababu ukarabati wenyewe hauonekani kama umefanyika.
Alisema kitendo hicho kinapelekea kurudisha nyuma kasi ya maendeleo ya halmashauri hiyo na kueleza kwa maslahi yake inabidi soko hilo livunjwe lakini mchakato huo uendane na kuwashirikisha wataalamu ili waweze kuamua nini kifanyike.

Samaki wakiwa Mezani kwa Mauzo
Diwani huyo alisema lazima madiwani wahakikishe wanakuwa mstari wa mbele kusimamia maslahi ya wananchi wanaowaongoza ili kuondoa kero zao lengo likiwa ni kuwapa maendeleo.

  “Kila mwaka zilikuwa zikitengwa milioni 50 kwa ajili ya ukarabati wa soko hilo lakini watu walikuwa hawazisema ila hizo milioni 11 kwa ajili ya kupewa mtathimini zimekuwa zikileta maneno naamini wataalamu tunao kwenye halmashauri waamue nini cha kufanya pale lakini hilo soko bora livunjwe “Alisema Gadafi.

Hivi ndivyo samaki wanavyouzwa katika soko hilo
Akizungumza suala hilo,Mjumbe wa Kamati wa Fedha,Shehe Fadhili Bwanga alisema masuala ya kuvunjwa soko hilo ni kutokana na kuona kuwa halikidhi haja ya kuendana na hadhi ya jiji na wao kupitia kamati ya fedha wameona zifuatwe sheria za nchi ikiwemo kuthaminiwa na kampuni zinazotambulika kiserikali ili ziweze kutoa idhini ya uvunjwaji wa jengo hilo.

Bwanga aliongeza kuwa uamuzi wa kuvunja soko hilo pia utatokana na gharama zake za sh.milioni 11 lakini sheria za uvunjwaji zilizowekwa inabidi zifuatwe kabla ya kuachukua maamuzi wa uvunjwaje wake.

No comments:

Post a Comment