HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 7 January 2016

RANGI YA MKOJO WAKO INA MAANA GANI KWA AFYA YAKO? SOMA HAPA UJUE.



Habari ndugu msomaji wa makala hii,napenda kukushukuru kuungana nami katika makala hii kutoa elimu juu ya kuepukana na magonjwa mbalimbali.
Rangi ya mkojo hubadilika kutokana na kiasi cha maji kilichopo mwilini mwako.Rangi hizo ni;
1. Mweupe kabisa (Usio na Rangi):
Hii inaashiria kuwa unakunywa maji mengi kupita kiasi. Ikiwezekana unashauriwa upunguze kidogo
2.Rangi njano iliyochanganyika na Kijani kidogo: Ni kawaida,na inaonyesha kuwa una afya na Mwili wako una maji ya kutosha.
3. Njano iliyopauka:
Upo kawaida tu. Endelea kunywa maji ya kutosha.
4. Njano iliyokolea:
Upo kawaida lakini unashauriwa kunywa maji ya kutosha.
5. Njano inayokaribia kufanana na Kahawia au Rangi kama ya Asali:
Hii ni ishara kuwa mwili wako hauna maji ya kutosha, hivyo unshauriwa kunywa maji kwa wingi sasa.
6. Rangi ya Kahawia:
Huenda una matatizo kwenye Ini lako au upungufu mkubwa wa uaji mwilini. Kunywa maji ya kutosha na umwone daktari kama hali hii ikiendelea.
7. Rangi ya Pinki inayokaribia kuwa kama Nyekundu:
MIKE L.CHIKOMA
Mshauri wa afya.
Kama hujala matunda yoyote yenye asili ya wekundu, basi huenda una Damu kwenye kibofu chako cha mkojo. Lakini inaweza ikawa ishara ya ugojwa wa Figo, uvimbe, matatizo kwenye njia ya mkojo, au matatizo kwenye kibofu. Muone daktari haraka iwezekanavyo.

-KUNYWA MAJI MENGI NA YA KUTOSHA KILA MARA KWA AFYA BORA YA MWILI WAKO.MAJI NI DAWA YA BURE TULIPEWA NA MWENYEZI MUNGU,LAKINI TUNASHINDWA KUITUMIA,ANZA SASA KUITUMIA UONE FAIDA ZAKE!KWA USHAURI NA MAELEZO ZAIDI,WASILIANA NAMI KUPITIA 0713671316 & 0788671516-calls,sms & whatsap

No comments:

Post a Comment