HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 11 January 2016

LEO NI SIKUKUU YA MAPINDUZI.



WAZANZIBARI leo wanasherehekea miaka 52 ya Mapinduzi ya Januari 12 mwaka 1964, ambayo yaling’oa utawala wa Sultani kutoka Oman na kuwezesha wazalendo wengi kushika hatamu ya kuongoza nchi.
Katika kilele cha sherehe hizo, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk Ali Mohamed Shein atahutubia taifa katika uwanja wa Amaan.

Atapokea maandamano ya wananchi wa mikoa mitano ya Unguja. Matukio mengine makubwa yatakayofanyika katika uwanja huo ni Rais Shein kukagua gwaride la heshima la vikosi ya ulinzi na usalama, vikiongozwa na Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) .

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na idara ya sherehe na mapambo iliyo chini ya Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais, sherehe hizo zitahudhuriwa na viongozi wa ngazi za kitaifa akiwemo Rais wa Jamhuri ya Muungano, John Magufuli ambaye ni mara ya kwanza kushiriki baada ya kuchaguliwa katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 25 mwaka jana.

Ratiba hiyo inaonesha kwamba sherehe hizo, zitahudhuriwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa na marais wastaafu wa Jamhuri ya Muungano na wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Akizungumza na waandishi wa habari, Makamu wa Pili wa Rais, Balozi Seif Ali Iddi aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi kusherehekea miaka 52 ya Mapinduzi, yaliyowakomboa wakulima na wafanyakazi kutoka katika kucha za wakoloni wa kisultani.Aliwapongeza wananchi kwa kujitokeza na kushiriki katika ufunguzi wa miradi ya maendeleo, ambayo malengo yake ni kuharakisha maendeleo na kupambana na umasikini.

Mitaa mbalimbali mjini Zanzibar, imepambwa picha za viongozi mashuhuri waliosimama kidete kufanya Mapinduzi hayo; hususan Rais wa Kwanza, Abeid Amaan Karume aliyeongoza timu ya watu 16 kufanya mapinduzi hayo.Mmoja wa walioshiriki kwenye mapinduzi, Hamid Ameir (82) , alieleza kufurahishwa na jinsi malengo ya Mapinduzi ya mwaka 1964 yanavyotekelezwa kwa vitendo.

No comments:

Post a Comment