HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 12 January 2016

NSSF WATOA MSAADA WA MASHUKA 100 KWA ZAHANATI YA KWEDIBOMA, KILINDI MKOANI TANGA.



Kilindi, MFUKO wa Hifadhi ya Jamii (NSSF) Tawi la Korogwe Mkoani Tanga limetoa msaada wa mashuka 100 kwa Zahanati ya Kwediboma Wilayani hapa kujikinga na baridi kwa wagongwa wanaolazwa kituoni hapo.
Akizungumza mara baada ya makabidhiano, Kaimu Meneja NSSF tawi la Korogwe,  Rebule Maira, alisema msaada huo ni moja ya misaada inayotoa kwa wateja wake vikiwemo vituo vya Afya na shule.
Alisema NSSF ilipata taarifa za  kituo  kukabiliwa na uhaba wa mashuka kwa wagonjwa wanaolazwa na hivyo mfuko kuona umuhimu wa kukisaidia na  kuweza kukabiliana na changamoto mbalimbali za wagonjwa.
Mfuko wa hifadhi ya jamii uko kwa ajili ya jamii na leo ndio maana tumekuja hapa kusaidia jamii, tumetoa mashuka kwa ajili ya wagonjwa kujikinga na baridi kali kama tujuavyo wilaya hii iko na baridi kali” alisema Rebule na kuongeza
“Mfuko uko na utaratibu wa kusaidia jamii ambapo hutenga fungu maalumu kama ujenzi wa maabara na shule pamoja na huduma nyenginezo niwahaakikishie wananchi lengo letu nikusaidia  jamii” alisema
Kwa upande wake mkuu wa kituo ambaye pia ni muuguzi kituo cha Zahanati Kwediboma, Sister Matilda Pitter, amesema kituo hicho kinakabiliwa na changamoto nyingi zikiwemo uhaba wa vitanda kwa wagonjwa na majengo.
Alisema kituo hicho kimekuwa kikipokea wagonjwa wengi na baadhi yao kutoka Handeni na Songe pamoja na vijijini hivyo kuyataka mashirika ya umma na Serikali kukisaidia na kuiga mfano wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii NSSF.
Alisema kituo kimekuwa kikipokea wagonjwa wengi tofauti na uwezo wake na hivyo kutaka kuongeza majengo ambayo yatakuwa na uwezo wa kupokea wagonjwa wengi wanalazwa.
“Zahanati yetu inakabiliwa na changamoto nyingi ikiwemo uhaba wa majengo ambapo kwa sasa ndio kama unavyoona majengo tunayojenga , changamoto iko katika umaliziaji” alisema Matilda
Matilda ameitaka mifuko mengine  ya Hifadhi ya Jamii na mashirika na Serikali kukisaidia kituo hicho ili kuweza kuwapatia wananchi huduma ya matibabu na kuondosha kero ya kufuata matibabu masafa marefu.
CHANZO:TANGA KUMEKUCHA BLOG

No comments:

Post a Comment