Habari ndugu msomaji wa makala hii napenda kukushukuru kwa kuungana nami katika makala hii kutoa elimu juu ya kuepukana na magonjwa mbalimbali.
KWA KUTUMIA VITU ASILIA KABISA.
Shinikizo la damu(presha) ni tatizo la siku nyingi ambalo lilikuwa likiwapata watu wenye umri mkubwa, lakini leo hii takriban asilimia 30% ya vijana duniani wanakabiliwa na tatizo hili.
Zaid ya watu billion moja duniani wanakumbwa na tatizo, ugonjwa huu ni hatari sana kwani husababisha madhara makubwa kwa mwanadamu ikiwemo;
1.Mshituko wa moyo (heart attack )
2. Kiharusi (stroke)
3. Kupanuka kwa moyo na hatimaye kufeli na mengineyo.
Madhara haya ni makubwa na yamepelekea watu wengi kuaga dunia.
Kwa kutambua madhara yatokanayo na ugonjwa huu,nimeamua kutumia muda wangu kuandika makala hii kwa ajili yako ndugu msomaji.
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEi6M_4t28xz1CHKtcG7qVzOnoo7NmYtM-czlMJ5EyUf6tQi1OCevd2tPOtbtuXjggmMswrNuSmwb7gzhGpaGJCLTDSX_AidoIEj_ZCfJObwGG9j07FndxUgx6AstPVA-yowwJKLhzgZ9pS4/s320/12369239_519308584912940_4819840350293383787_n.jpg)
Njia hizi kumi (10) zitakusaidia kudhibiti presha yako na kufanya uishi mda mrefu.
Zifuatazo ni njia kumi za kudhibiti presha au shinikizo la damu kwa kutumia vitu asilia visivyo na madhara kabisa kwa mtumiaji.
1. Tambua kiwango cha presha yako.
Hiki ni kitu cha kwanza unachotakiwa ukifanye kwani watu wengi hatuna utaratibu wa kupima presha zetu, kwa hiyo inabidi upime na kujua kiwango cha presha yako.
Presha hupimwa kwa namba mbili mfano 120/80 ambapo namba ya juu (SBP) huonesha kiwango cha presha kinachotoka kwenye moyo kuingia kwenye mishipa ya damu
Namba ya chini (DBP) huonesha kiwango cha presha ambacho hutumika kupeleka damu katika ventriko ya kushoto UCHAMBUZI WA PRESHA:
1. Kawaida ni chini ya 120
2. Hatari ya kupata (120-139)
3. Presha daraja 1 (140-159)
4. Presha daraja 2. (zaidi ya 160)
Kwa hiyo ni vema ukatambua uko ktk kundi gani Kati ya hayo manne.
2. Tumia vyakula vitokanavyo na mimea:
Vyakula hivi huwa na mafuta kidogo na hivyo hukupa afya nzuri ya moyo na mishipa ya damu, tafiti zinaonesha utumiaji wa vyakula vitokanavyo na mimea hupunguza presha kwa kiwango cha 7/5 mmhg
vyakula hivi nimevigawa katika makundi manne kama ifuatavyo;
1. Nafaka
2. Mboga mboga
3. Jamii ya kunde
4. Matunda
Ukitumia vizuri makundi haya ya vyakula basi utaweza kudhibiti presha yako.
3. Punguza kiasi cha chumvi:
Mtu mzima anahitaji <1500mg za chumvi kwahiyo jaribu kupunguza kiwango cha chumvi kwani figo hutumia chumvi (sodium) kama njia ya kupandisha presha.
4. Kula vyakula vyenye potassium kwa wingi
Unapotumia vyakula hivi mwili hupata kiwango kikubwa cha potassium, mtu mzima anahitaji 4700mg za potassium kila siku ili kuweza kupunguza presha mwilini, kwani figo hutumia potassium kushusha presha mwilini.
VYAKULA VIPI VINA POTASSIUM??
vyakula kama ndizi, nyanya na bidhaa zote zitokanazo na nyanya, machungwa, mboga za majani, maharage nk.
5. Mazoezi:
Tenga mda wa dakika 30 kwa siku kwa ajili ya mazoezi, mazoezi husaidia kupunguza uzito na kusafisha mfumo wa damu hivyoo basii husaidia katika kushusha presha yako.
6. Punguza uzito:
Uzito mkubwa ni chanzo cha magonjwa mengi yakiwemo magonjwa ya moyo kama Vile presha hivyo basi punguza uzito wako kuepukana na tatizo hili.
7. Punguza utumiaji wa pombe.
Pombe ikitumiwa kwa kiwango kidogo ni nzuri kwa afya mfano mwanamke anashauriwa atumie chupa moja tu kwa siku ( hatari ya kupata kansa ya matiti) na mwanamme atumiee angalau chupa mbili kwa siku
Pombe kupita kiasi husababisha mafuta mabaya (LDL) kwenda kudeposit kwenye mishipa ya damu na kufanya kupungua kwa ukubwa wa mishipa ya damu na kupelekea mtu kupata presha.
8. Epuka uvutaji sigara au tumbaku:
Kwani uvutaji sigara humuweka mtu katika nafasi ya kupata magonjwa ya moyo Mara mbili zaidi ya yule asiyevuta.
9. Punguza msongo wa mawazo:
Unapokuwa na msongo wa mawazo mwili hutoa homoni za adrenaline na cortisol ambazo hufanya mishipa ya damu kusinyaa na kufanya damu kusafiri kwa kasi kubwa na hatimaye hupelekea mtu kupata presha.
10. Matumizi ya dawa asilia zisizo na kemikali.
Kwa wale wote ambao hushindwa kupunguza presha zao kwa kutumia njia hizo 9 hapo juu au ni wagonjwa wa siku nyingi huwa nawashauri watumie dawa asilia kabisa iliyotengenezwa kutokana na mmea wa Ginkgo na kuwekwa kitaalamu katika mfumo wa vidonge;
![](https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEjijzFN44YmZ2hyKVVCEY87kMMBDX3E1jmytCSVN3xP25nH7yyPwT4CRK34mx2s6SrU7mVwYAsVDDdMmMtPEzGMU7xGhOarUrWxs3_MpeyhN2jUGUppJkNpSsIPPgNvHsTZAoB5f2VeLHXz/s320/12346479_519308551579610_1804833803237021761_n.jpg)
DAWA HII INA KAZI ZIFUATAZO:
1. Huondoa mafuta na mabaki kwenye mishipa ya damu,
2. Huondoa oksijeni iliyoshindwa kutumika kwa mabaki haya ya hewa hii ni chanzo kikubwa cha presha na kansa mbalimbali.
3. Humkinga mtu asipate madhara yatokanayo na presha,
4. Huzuia damu isigande ktk mishipa,
5. Huzuia utengenezaji wa mabonge kutoka kwenye damu iliyoganda ambayo ndio chanzo kikubwa cha kiharusi (stroke )
6. Husaidia kubalance damu inayokwenda kwenye moyo na ubongo.
KWA USHAURI NA MAELEZO ZAIDI
WASILIANA NAMI KUPITIA NAMBA 0713671316 & 0788671516-call/sms/whatap
IMEANDALIWA NA MIKE CHIKOMA,
Mshauri wa Afya.
IMEANDALIWA NA MIKE CHIKOMA,
Mshauri wa Afya.
No comments:
Post a Comment