HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 22 December 2015

WANANCHI HANDENI WALIA NA SERIKALI KUFUATIA UONGOZI WA KIJIJI KUUZA ZAIDI YA HEKTA 250 ZA MSITU .



Wakazi zaidi ya 2000 wa kijiji cha Magamba kilichopo kata ya Kwaluguru wilayani Handeni wameiomba serikali kuingilia kati kufuatia viongozi wa serikali ya kijiji hicho kuuza hekta zaidi ya 250 za msitu wa hifadhi ya asili kijijini hapo kwa wawekezaji ambao wamejitambulisha kuwa ni familia ya rais mstaafu wa Zanzibar Dr, Salmin Amoury.

Wakizingumza katika kijiji cha Magamba baadhi ya wakazi hao wamesema afisa wa serikali ya kijiji hawashirikisha wananchi wala idara ya misitu wakati alipofanya zoezi hilo na badala yake ameshirikiana na viongozi wa kamati ya ardhi ya kijiji kisha kuuza eneo hilo bila kuzingatia sheria na taratibu zilizowekwa.
Hata hivyo mwenyekiti wa serikali kijiji cha Magamba Bwana Salum Gumbo akielezea sakata hilo amesema yeye hakushirikishwa na afisa mtendaji wake wa kijiji Erick Semsela kwa sababu baada ya wananchi kuitisha kikao cha kujadili suala hilo alikimbia kijijini hapo na kwenda kusikojulikana.

Kufuatia hatua hiyo msemaji wa familia ya rais mstaafu Bwana Munir Juma Amoury ameziomba mamlaka husika kuchukua hatua za makusudi kwa sababu walilipa fedha zao kwa mtendaji wa serikali ya kijiji hicho wakiamini kuwa maeneo hayo ni salama kumbe ni hifadhi ya misitu ya asili.
SOURCE:ITV

No comments:

Post a Comment