HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 23 December 2015

"JIPU JINGINE" WAZIRI MKUU AFUTA HATI YA SHAMBA LA MKONGE LA AMBONI MKOANI LINDI.



Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetangaza kufuta hati miliki ya shamba la mkonge la Kikwetu mkoani Lindi baada ya mmiliki wake kampuni ya Amboni Estates Ltd kushindwa kuliendeleza hadi sasa.

Kwa mujibu wa  Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa wakati akizungumza na  wakazi wa Lindi alisema serikali imechukua hatua hiyo kufuatia kushindwa kuliendeleza ambapo  shamba hilo  litakuwa  kuwa chini ya serikali.

Aidha, Shamba hilo linalodaiwa kupewa hati ya umiliki wa miaka 99 na baadaye kampuni ya Tasco kabla ya kuchukuliwa na Mohamed Enterprieses Tanzania Ltd lilikuwa likizalisha mkonge kwa ajili ya kutengeneza magunia.

Katika mkutano huo  Majaliwa alisema tayari shamba hilo lipo huru na kampuni ya BSG ipo huru kujenga mitambo itakayotumika kusafishia gesi asilia kwenye eneo hilo.
Akizungumzia   uendelezwaji wa kiwanda cha kuzalisha saruji cha Meis ambacho ujenzi wake umesimama kwa muda kutokana na sababu mbalimbali zikiwamo za kisiasa, Majaliwa alisema kazi hiyo inatarajiwa kuanza tena muda mfupi ujao baada ya kupatikana kwa wataalam.

Kwa upande mwingine Majaliwa alisema  kujengwa kwa viwanda ndani ya mji huo, kutasaidia kupunguza tatizo la upatikanaji wa ajira kwa wananchi wa Mkoa wa Lindi na vitongoji vyake.

No comments:

Post a Comment