HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 4 December 2015

MKUU WA MKOA TANGA AKERWA NA UCHAFU WA MAZINGIRA MKOANI HUMO.



MKUU wa Mkoa wa Tanga, Mwantumu Mahiza (Pichani) amesema haridhishwi na kiwango cha usafi wa mazingira katika mitaa ya jiji la Tanga licha ya halmashauri hiyo kupongezwa kwa kushika nafasi ya pili kwa usafi hapa nchini.

Ametoa kauli hiyo jana wakati akihoji kuhusu baadhi ya mambo aliposomewa kutoka kwenye taarifa ya maendeleo ya wilaya ya Tanga wakati wa ziara yake ya kikazi jijini humo.

Katika taarifa hiyo iliyosomwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga, Abdula Lutavi alisema kwa miaka miwili mfululizo sasa jiji hilo limefanikiwa kushika nafasi ya pili kitaifa kwa usafi kutokana na kazi nzuri inayofanywa na wananchi kwa kushirikiana na vikundi 10 ambavyo vimeajiri vijana 110.

Mahiza alisema pamoja na jitihada hizo bado kuna baadhi ya maeneo ya mji wa Tanga ni machafu, yananuka na mifereji imejaa taka ngumu za mifuko ya plastiki. “Niwe mkweli tu nitamke kwamba mitaa ya Tanga bado ni michafu, masoko machafu, mifereji imeziba makazi ya watu ni machafu ki msingi bado sijaridhishwa na usafi kwa sababu kipindupindu kipo hapa.

Usafi huo mmeupata wapi acheni kulewa sifa safisheni mji “ alisema. Aidha Mkuu huyo wa Mkoa aliutaka uongozi wa halmashauri ya jiji hilo kuitumia sheria kukataza matumizi ya mifuko ya plastiki ambayo inaongoza katika uchafuzi wa mazingira.

No comments:

Post a Comment