HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Monday, 28 December 2015

BREAKING NEWSSS..!! YANGA YAVUNJA MKATABA NA NIYONZIMA "YAMDAI FIDIA YA DOLA ELFU 17"


YANGA SC imevunja Mkataba na kiungo wa kimataifa wa Rwanda, Haruna Hakizimana Fadhil Niyonzima kutokana na mchezaji huyo wa Amavubi kukiuka vipengele.

Katibu Mkuu wa Yanga SC, Dk Jonas Tiboroha (Pichani Kushoto) amewaambia Waandishi wa Habari katika Mkutano uliofanyika makao makuu ya klabu, Jangwani, Dar es Salaam mchana wa leo kwamba  Haruna pia atatakiwa kuilipa klabu fidia dola elfu 71 kwa kukiuka mkataba.

Niyonzima aliwahi kuwasilisha vielelezo vyote vya kumsafisha na kubatilisha adhabu aliyopewa Yanga SC.
Niyonzima alifungiwa kwa muda usiojulikana Yanga SC wiki tatu zilizopita kwa tuhuma za utovu wa nidhamu baada ya kuchelewa kurejea klabuni, kufuatia ruhusa ya kwenda kuichezea timu yake ya taifa kwenye Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge nchini Ethiopia mwezi uliopita.

Hata hivyo, baada ya kuchelewa alirejea akiwa amefungwa plasta gumu (PoP) na kusema aliumia kwenye mashindano hayo, hivyo akabaki Kigali kupata matibabu.

Lakini hiyo haikumsaidia kumuepusha na adhabu ya uongozi wa Yanga SC uliokuwa na hasira naye, ukidai imekuwa desturi yake kuchelewa kila anaporuhusiwa kwenda kwao.

Pamoja na hayo, Niyonzima amewasilisha vielelezo vya barua pepe alizokuwa akituma kwa Katibu Mkuu wa Yanga SC, Dk Jonas Tiboroha ambaye kwa bahati mbaya alikuwa hajibu.

Amewasilisha pia ushahidi wa vyeti vya Daktari wa timu ya taifa na barua ya Shirikisho la Soka Rwanda (FERWAFA) vyote vikithibitisha kweli aliumia na alibaki kwa matibabu Kigali.  
TAARIFA ILIYOTOLEWA NA YANGA LEO
 
 

No comments:

Post a Comment