HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 20 December 2015

BREAKING NEWSS...GUARDIOLA OUT.. ANCELOTTI IN >>BAYERN MUNICH



MABINGWA wa Bundesliga huko Germany, Bayern Munich, wametangaza kuwa Kocha wa zamani wa Real Madrid na Chelsea, Carlo Ancelotti, ndie atakuwa Kocha wao mpya kwa Msimu ujao.Kocha wa sasa, Pep Guardiola, anatarajiwa kujiunga na Manchester City ingawa hili bado kuthibitishwa na anabaki pia kuhusishwa na Man United na Chelsea.

Hata hivyo, Kocha huyo wa zamani wa Barcelona mwenye Miaka 44 ana nafasi kubwa kutua Etihad hasa kutokana na urafiki wake wa karibu na Mkurugenzi wa Soka wa CitY Txiki Begiristain pamoja na Mtendaji Mkuu Ferran Soriano, Watu ambao alikuwa nao Barcelona.

Mwezi Agosti, Man City ilimwongezea Meneja wao wa sasa, Manuel Pellegrini, Mkataba wa Mwaka mmoja zaidi hadi Juni 2017 lakini hilo linaonekana si tatizo kwa Guardiola kumbadili.Guardiola alijiunga na Bayern Munich Mwaka 2013 na kutwaa Ubingwa wa Bundesliga kila Msimu na safari hii pia yuko njiani kuutwaa kwa mara ya 3 mfululizo.

Akiwa na Barcelona, kwa Miaka Minne, Guardiola aliweza kuiongoza kutwaa La Liga mara 3 na UEFA CHAMPIONZ LIGI mara 1.Carlo Ancelotti, ambae amekuwa hana kibarua tangu Msimu uliopita alipoondolewa Real Madrid, amesaini Mkataba wa Miaka Mitatu na Bayern Munich.

No comments:

Post a Comment