HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Sunday, 20 December 2015

BARCELONA MABINGWA WA DUNIA.. SUARES & MESSI KIBOKO YAO...!!!



MABINGWA wa Ulaya, FC Barcelona, Leo wamebeba Kombe la Dunia kwa Klabu huko International Stadium Yokohama, Jijini Yokohama, Japan baada ya kuifunga River Plate ya Argentina Bao 3-0.
Hili ni Kombe la 5 kwa Barca kutwaa kwa 2015 baada ya kuyazoa La Liga, UEFA CHAMPIONZ LIGI, Copa del Rey na lile la Ulaya la Super Cup na hili ni Kombe lao 3 la Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu.Bao za Barca zilifungwa na Lionel Messi, na kudumu hadi Haftaimu, na nyingine za Kipindi cha Pili za Luis Suarez.

Katika Mechi ya awali ya kusaka Mshindi wa 3, Wenyeji Sanfrecce Hiroshima walitoka nyuma na kuipiga Guangzhou Evergrande Bao 2-1.Magoli ya Sanfrecce Hiroshima yalifungwa na Douglas katika Dakika za 70 na 83 wakati lile la Guangzhou Evergrande lilipachikwa katika Dakika ya 4 na Paulinho.
 MABAO YA BARCELONA LEO YAMEFUNGWA NA LIONEL MESSI NA LUIS SUAREZ AMBAYE ALIPIGA BAO MBILI.
VIKOSI:
River Plate: Barovero, Mercado, Maidana, Balanta, Vangioni, Kranevittter, Ponzio, Sanchez, Viudez, Mora, Alario
Akiba: Chiarini, Batalla, Vega, Casco, Mammana, Mayada, Martínez, L Gonzalez, Pisculichi, Bertolo, Driussi, Saviola
Barcelona: Bravo, Alves, Pique, Mascherano, Alba; Busquets, Iniesta, Rakitic, Neymar, Suarez, Messi
Akiba: Ter Stegen, Masip, Douglas, Bartra, Munir, Sandro, Roberto, Adriano, Vermaelen, Mathieu, Samper, Gumbau
REFA: Alireza Faghani [Iran]

No comments:

Post a Comment