HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 22 December 2015

BOMOA BOMOA MSIMBAZI YASITISHWA HADI 2016.



Serikali kupitia wizara ya Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Baraza la Taifa la Hifadhi ya Usimamizi Mazingira (NEMC) kwa kushirikiana na Halmashauri za Manispaa za  jiji la Dar es salaam wametangaza kusitishwa kwa muda zoezi la bomoa bomoa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa leo na Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi imebainisha kuwa  zoezi la bomoa bomoa limesimamishwa kwa muda kuanzia tarehe 22,12,2015 hadi 05,01.2016.

Taarifa hiyo imeongeza kuwa eneo la mto msimbazi ni eneo hatarishi na ujenzi katika eneo hilo ni kinyume na sheria ya mipango miji na 8 ya mwaka 2007 na sheria ya mazingita na.4 ya mwaka 2004.

Maeneo mengine ambayo serikali imepiga marufuku ni maeneo ya wazi, kingo za mito, fukwe za bahari, maeneo ya hifadhi za barabara na maeneo hatarishi.

Aidha, kwa hapa Dares salaam maeneo ya wazi  takribani 180 yamevamiwa ambayo ni kama ifuatavyo; Halmashauri ya wilaya ya Kinondoni  maeneo 111,  Halmashauri ya Ilala maeneo 50 na Halmashauri ya Temeke maeneo 19.

No comments:

Post a Comment