HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 29 July 2015

WAVUVI WILAYANI PANGANI WALILIA MAFUNZO YA UJASIRIAMALI NA UVUVI WA KISASA.



BAADHI ya wavuvi wa vijiji vya Ushongo na Stahabu wilayani Pangani Mkoani Tanga wanaiomba halmashauri ya wilaya hiyo kuwapatia mafunzo maalum yatakayojengea stadi na uwezo wa kuanzisha vikundikazi katika shughuli zao.

Wametoa ombi hilo kwenye hafla ya kufunga mafunzo ya wiki moja kwa sekta isiyo rasmi kuhusu uvuvi endelevu, mafunzo yaliyoendeshwa na Mamlaka ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi Stadi (VETA) Kanda ya Kaskazini.

Ramadhani Seif mvuvi kutoka kijiji cha Stahabu amesema mafunzo aliyopata kuhusu uvuvi endelevu na ujasiriamali anaamini yatamletea tija zaidi endapo hasa halmashauri itawawesha wavuvi kuunda vikundi vya uzalishaji mali.

Pia Mwahija Silaha mvuvi wa kijiji cha Ushongo amesema utekelezaji wa hatua hiyo utawakwamua ki uchumi kwa kuwezesha kufanya uvuvi endelevu na hivyo kuondokana na hali duni ya maisha kwenye kaya.

Kwa upande wake Mkurugenzi wa VETA Kanda ya Kaskazini, Angelus Ngonyani amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha kutambua sera na sheria za wavuvi na hatimaye kufanya shughuli zao kwa usahihi na kujikwamua kiuchumi kwa kuongeza kipato katika jamii.

Awali akifunga mafunzo hayo yaliyoshirikisha wavuvi na wajasiriamali 90 Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Pangani, Melea Mkongwa amewataka washiriki kuzingatia stadi walizopata kwa kujiepusha na uvuvi haramu.

No comments:

Post a Comment