HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 29 July 2015

HABARI NJEMA KUTOKA HOSPITALI YA MKOA BOMBO TANGA. UPASUAJI WA BURE.



Hospitali ya Mkoa Bombo kwa kushirikiana na Madaktari wa Shirika la Interplast la Ujerumani inatazamia kutoa huduma ya bure  ya upasuaji wa kurekebisha maumbile kama kupasuka midomo ( cleft lips) kupasuka kaakaa (cleft palate) Uvimbe ( turmors) na Makovu sugu ambayo itakuwepo kwa muda wa siku 10.
Huduma ya upasuaji imeanza kwa uchunguzi wa wagonjwa wenye matatizo hayo kisha kupangiwa tarehe ambapo uchunguzi wa awali unaanza tarehe 3/08/2015 zoezi litakalo dumu kwa majuma mawili.

Kwa mujibu wa mratibu wa zoezi hilo la upasuaji Dr Wallace Karata, amesema ushirikiano wa upande hizi mbili katika kunusuru maisha ya Watanzania ulianza  mwaka 2011 ambapo hospitali iliona umuhimu wa kuwasaidia wananchi hasa wale wasio na uwezo wa kulipia upasuaji na matibabu.

Aidha, uandikishwaji wa wagonjwa wenye matatizo mbalimbali unagharimu shillingi za kitanzania elfu tano (5000) na zaidi ya watu 150 wamejitokeza kufanyiwa uchunguzi wa awali kwa ajili ya upasuaji huo.

No comments:

Post a Comment