HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 29 July 2015

MBWANA SAMATTA AGOMA KUSAJILIWA NA ZAMALEK KWA BILIONI 2.3 MIPANGO NI ULAYA TU.



Mbwana Samatta ni mshambuliaji wa kimataifa kutokea Tanzania anaeichezea klabu ya TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo ambayo alijiunga nayo mwaka 2011 akitokea Simba ya Tanzania na mpaka sasa amekua mmoja kati ya wachezaji mahiri wanaounda safu imara ya ushambuliaji kwa TP Mazembe na timu ya taifa ya Tanzania.
Samatta aliingia kwenye headlines siku kadhaa zilizopita baada ya kukataa kusajiliwa na klabu ya Zamalek ya Misri kwa euro milioni 1 kutoka TP Mazembe ambayo ni sawa na zaidi ya bilioni 2.3 za Kitanzania, kila media iliandika hii story nakuonekana kama Samatta amepoteza bahati.

Wakala wa mchezaji huyo Jamal Kasongo amezungumzia suala hilo na mpango wa Samatta licha ya kupewa ofa ya mshahara mkubwa.
La kwanza ni kweli maafisa wa Zamalek wawili walifika kipindi mimi nipo na Mbwana kipindi yupo katika mechi ya timu ya taifa kimsingi mimi niliweza kukaa nao chini kuweza kufanya nao majadiliano lakini lazima mchezaji ili ufikie malengo uweze kukaa katika mstari, msimamo wa Mbwana na msimamo wangu mimi kama mshauri wake ni Mbwana kuweza kucheza Ulaya” alisema Jamal Kasongo

Wakatuma tena ofa wako tayari kumnunua TP Mazembe kwa euro milioni 1 na euro milioni 1 ni pesa nyingi na walikuwa tayari wakimuhitaji waweze kumpa mshahara ambao hakuna mchezaji ndani ya Afrika hii anaweza akalipwa lakini bado hili suala lilikuwa gumu kwani lengo kubwa ni Mbwana kucheza Ulaya” alisema Jamal Kasongo

Mbwana Samatta anamaliza mkataba wake na TP Mazembe mwezi April 2016 hivyo anaweza kuwa mchezaji huru na kuchagua timu ipi ya kwenda.

No comments:

Post a Comment