HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Tuesday, 9 February 2016

WAZIRI AMTAKA LOWASA KUTOA TAARIFA ZA MAGAIDI WA AL-QAEDA NCHINI.



WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Mohamed Aboud Mohamed amemtaka Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowassa (pichani)kutoa taarifa za kuwapo kwa tishio la kundi la al Qaeda kuingia nchini kwa vyombo vya ulinzi na usalama ili vyombo hivyo, vishughulikie hatari hiyo.

Katika mazungumzo yake na wanahabari hili, Aboud alisema kwa kuwa Lowassa anaelewa madhara ya ugaidi na ana taarifa za kina kuhusu kundi hilo, ni vyema akazipeleka kwenye vyombo vya usalama.
Mwishoni mwa wiki, Lowassa ambaye alikuwa mgombea urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) katika uchaguzi mkuu wa mwaka jana, alionya kuwa ipo hatari Zanzibar ikatumiwa kuwa njia ya kuingia magaidi wa aina ya Al-Qaeda nchini.

Lowassa alidai kuwa hilo linaweza kufanyika, endapo jitihada maalumu hazitafanyika sasa katika kumaliza mkwamo wa kisiasa visiwani humo na kuzuia uwezekano wa kuvunjika kwa hali ya amani.

Lakini, Waziri Aboud aliyewahi kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi katika Serikali ya Awamu ya Nne, alisisitiza kuwa Zanzibar ina amani na utulivu na kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imejipanga kuhakikisha hali ya utulivu na amani inaendelea kudumu.

Alisema SMZ itahakikisha inatekeleza agizo la Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) la kufanyia uchaguzi wa marudio na kuwapo kwa vitisho kutoka kwa baadhi ya vyama vya upinzani.

Zanzibar inatarajia kufanya uchaguzi wa marudio wa kuchagua Rais wa Zanzibar, Wawakilishi na Madiwani Machi 20, mwaka huu, baada ya ule uliofanyika Oktoba 25, mwaka jana kufutwa siku tatu baadaye kwa tangazo la Mwenyekiti wa ZEC, Jecha Salim Jecha kutokana na kuwapo kwa kasoro kadhaa.

ZEC ipo katika maandalizi ya matayarisho ya uchaguzi huo huku ikitoa matangazo kupitia vyombo vya habari kuwataka wananchi wenye sifa, kujitokeza kuomba nafasi mbalimbali ikiwemo za uandishi katika vituo vya kupiga kura.

Katika kilele cha maadhimisho ya miaka 39 ya kuzaliwa kwa CCM, yaliyofanyika Singida mwishoni mwa wiki iliyopita, Mwenyekiti wa Taifa wa CCM, Jakaya Kikwete aliwataka wanachama na wafuasi wa CCM Zanzibar, kujiandaa na uchaguzi wa marudio kwa ajili ya kukifanya chama hicho kuendelea na kushika dola.

No comments:

Post a Comment