HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Friday, 4 December 2015

CANNAVARO WA YANGA ATAJA MUDA WAKE WA MWISHO KWENYE SOKA.


‘Cannavaro’

Nahodha na beki wa kati wa Taifa Stars, Nadir Haroub ‘Cannavaro’, ametangaza rasmi kuwa, atastaafu kuichezea timu hiyo miaka mitatu ijayo.Kauli huyo, aliitoa jana Alhamisi mara baada ya kumalizika kwa mazoezi ya timu yake ya Yanga kwenye Uwanja wa Boko Veterani jijini Dar.

Mara baada ya Stars kufungwa na Algeria mabao 7-0, kuliibuka maneno kuwa Cannavaro na beki mwenzake wa kati, Kelvin Yondani, wanaonekana kuchoka kutokana na umri kuwatupa mkono.

Cannavaro ameliambia gazeti hili kuwa umri wake siyo mkubwa kiasi cha yeye kustaafu kuichezea Stars.

“Hizo kejeli na maneno ya watu nimeyazoea muda mrefu sana, kuhusiana na kiwango changu kushuka na umri kuwa mkubwa, hivyo ninachofanya ni kunyamaza tu.

“Muda wa kustaafu bado haujafika, nitafikiria hivyo miaka mitatu ijayo na tena nikistaafu hapo nitaendelea kuichezea Yanga, ikitokea nimeondoka Yanga basi jua kuwa ndiyo mwisho wangu wa soka umefika kwa sababu sifikirii kuichezea klabu nyingine mara baada ya hapo,” alisema Cannavaro ambaye ni nahodha wa Yanga.


TAMBWE AONGEZA MAJERUHI JANGWANI.
WAKATI kikosi cha Yanga kinatarajia kuingia kambini Jumatatu ijayo kujiandaa na michezo miwili ya Ligi Kuu Tanzania Bara itakayofanyika mkoani Tanga, mshambuliaji Amis Tambwe ameshindwa kuanza mazoezi kutokana na maumivu ya shingo.
 
Tambwe
Yanga itacheza mchezo wa raundi ya 10 dhidi ya Mgambo Shooting Desemba 12 mwaka huu Uwanja wa Mkwakwani Tanga, kisha siku chache baadaye itacheza na African Sports kwenye uwanja huohuo.

Akizungumza na gazeti hili jana, Kocha Mkuu wa Yanga Hans Pluijm alisema hadi kufika Jumatatu wachezaji wake wengi watakuwa wameunganika tayari kwa maandalizi kuelekea mchezo wao ujao.

Jana wachezaji wa Yanga waliendelea na mazoezi katika uwanja wa Boko Veterani, Dar es Salaam, lakini Tambwe aliyekuwepo mazoezini hapo alikuwa mtazamaji huku akiwa amefungwa kifaa tiba maalumu shingoni kutokana na matatizo ya shingo yanayomkabili.

Akizungumza na gazeti hili, Tambwe alisema huwa shingo wakati mwingine inamsumbua, ingawa si kwa kiwango cha kuogopa. “Lakini naamini nitakaa vizuri tu baada ya kupata matibabu,” alisema Tambwe.

Licha ya Tambwe, wachezaji Nadir Haroub ‘Cannavaro’, Haji Mwinyi na Oscar Joshua nao jana walishindwa kufanya mazoezi kutokana na majeraha yanayowakabili. Walifanya mazoezi mepesi kutokana na kuwa majeraha waliyopata wakiwa na timu ya Zanzibar katika mashindano ya Chalenji yanayoendelea nchini Ethiopia.

Joshua ameumia kifundo cha mguu. Akizungumzia hali zao daktari wa timu hiyo, Haruni Ally alisema zinaendelea vizuri na anatarajia pengine Jumatatu watakuwa wamepona na kujumuika kufanya mazoezi na wenzao isipokuwa Joshua.

“Wanaendelea vizuri, Cannavaro na Mwinyi wapo kwenye tiba na hali zao zinaendelea kuimarika na Tambwe shingo yake ina matatizo kidogo, lakini mpaka Jumatatu atakuwa kwenye mazoezi pamoja na wenzake isipokuwa Joshua yeye anaweza kuuguza kifundo kwa wiki mbili”, alisema Ally.

No comments:

Post a Comment