HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 21 May 2015

UANDIKISHWAJI KITAMBULISHO URAIA PONGWE "WANANCHI WATOA MAONI TOFAUTI"


Zoezi la kuandikisha vitambulisho vya Uraia linaendela kwenyevituo vya kata ya Pongwe ambapo wananchi wengi wanaendela kujitokeza kwa wingi kutimiza haki yao ya msingi.


Kituo cha Pongwe kaskazini kimekuwa na msongamano mkuibwa wa watu kulinganisha na vituo vingine ambapo kinamama na vijana wamekuwa wakitumia zaidi ya masaa saba kusubiri huduma hiyo hali inayoonesha jinsi gani zoezi hili limepokelewa vizuri na wananchi.

Akizungumza na mtandao huu Afisa Mtendaji wa kata ya Pongwe Bw Sali Mdoe amesema zoezi hilo linaendela vizuri kwani mashine zimegawanywa kwa kituo cha Pongwe kaskazini ili kurahisisha kazi kwa watendaji huku akipongeza wananchi kwa kujitokeza kwa wingi kweny vituo hivyo.
Mr Method Kapinga.

Mtandao huu umefanya mahojiano na baadhi ya wananchi waliofika kwenye kituo cha Pongwe kaskazini ambao wamekuwa na maoni tofauti juu ya zoezi hilo. 

Mr Moses Gasper
“Zoezi linaendela vizuri hakuna shida yoyote sisi Wazee tunahudumiwa kwa utaratibu tofauti na vijana jambao ambalo ni zuri na linaondoa usumbufu kwenye kituo hiki” Alisema mzee mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Mr Method Kapinga.

“Kwa upande wangu sijaridhishwa kabisa na mwenendo wa zoezi hili, nimefika hapa tangu saa 12 asubuhi na sasa ni saa saba mchana bado sijapata haki yangu ya kuandikisha, mimi nimejiajiri mwenyewe sasa muda wote huu niko hapa kazi nitafanya saa ngapi? Alisema mwananchi mwingin alijitambulisha kwa jina la Moses Gasper.

Moses alimalizia kwa kuitaka Serikali kuthamini muda wa wananchi wake ambao wengi hawana ajira kwa kufanya maandalizi ya kutosha kabla ya kuendesha zoezi kama hili ambapo ni muhimu kwa wananchi.
 

No comments:

Post a Comment