HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Thursday, 21 May 2015

LIGI YA HAMASA CUP PONGWE "HOME GUARD WAENDELEZA UBABE KWA COFFEE FC"




Kikosi cha Coffee fc
Ligi ya Hamasa Cup imeendelea leo kwa Mchezo mmoja mkali ambapo Home Guard Fc walipambana na Coffee fc katika Dimba za Ziwani kata ya Pongwe jijini Tanga.

Katika mchezo huo timu ya Home Guard imeendeleza ubabe mbele ya vijana wa Cofee kwa kuwachapa bao 1-0, mchezo uliojaza mashabiki wengi kutoka maeneo mbalimbali ya jiji kutokana na mvuto wa historian na mahusiano ya timu zote mbili.
Bao hili ya Home Guard limefungwa na Kombo Salehe dk ya 43 ya mchezo akimalizia mpira uliotemwa na golikipa wa Coffee alipopangua shuti la mshambuliaji wa Home Guard.
Kama kawaida Coffee fc imeendela kucheza soka  lake la pasi nyingi na kasi lakini bado tatizo la umakini na upangaji mzuri wa mashambilizi ni kikwazo kwa timu hiyo kupata ushindi.

Ligi hiyo itaendela kesho kwa mchezo mmoja utakaopigwa katika uwaja huohuo ambapo Middle Age watapambana na Bamba Ngumu fc.
Mchezo wa jana Young Rovers waliiburuza timu ya Pongwe Shooting bao 6-2 kikiwa ni kipigo kikubwa zaidi kweye ligi hiyo mpaka sasa.

No comments:

Post a Comment