HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA

HII NI KWA MARA YA KWANZA JIJINI TANGA
Tangaza biashara yako sasa uwafikie wateja wako kwa haraka na kwa gharama nafuu kupitia mfumo wa kisasa wa Digital Display Advertisement. Kupitia mfumo huu wateja wako watapata fursa ya kuona huduma zako na taarifa zote muhimu kupitia luninga kuwa za kisasa.

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA

KIJIWE KIPYA CHA BURUDANI JIJINI TANGA
MPANGO MZIMA WA KULA BATA UKO HAPA

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...

....HABARI NJEMA KWA AFYA YAKO...
.....tumia fursa yako vizuri....

Wednesday, 2 April 2014

>>UEFA CHAMPIONZ LIGI:RONALDO AIFIKIA REKODI YA MESSI BAO 14 MSIMU MMOJA UEFA CHAMPIONZ LIGI! CHELSEA YAPIGWA 3-1 NA PSG!

Cristiano Ronaldo


>>RONALDO AIFIKIA REKODI YA MESSI BAO 14 MSIMU MMOJA UEFA CHAMPIONZ LIGI!
Real Madrid, wakicheza Uwanjan kwao Santiago Bernabeu Jijini Madrid Nchini Spain, Usiku huu wameichapa Borussia Dortmund Bao 3-0 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.
Gareth Bale ndie aliefunga Bao la Kwanza katika Dakika ya 3 tu baada kuunganisha pasi safi ya Daniel Carvajal na kumzidi akili Kipa Roman Weidenfeller
Bao la Pili la Real lilifungwa katika Dakika ya 27 kupitia Isco kwa Shuti la chini toka Mita 20.

Hadi Mapumziko Bao zilikuwa Real 2 Dortmund 0.

Katika Dakika ya 57, Mchezaji Bora Duniani, Cristiano Ronaldo, alipiga Bao la 3 baada kumtoka Kipa Roman Weidenfeller kufuatia kupokea pasi safi ya Luka Modric.

Hilo ni Bao la 14 kwa Ronaldo kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu huu na ameifikia Rekodi ya Ronaldo ya Lionel Messi aliefunga Bao 14 katika Mechi 11 za UEFA CHAMPIONZ LIGI Msimu wa 2011/12 wakati Ronaldo amechukua Mechi 8 tu.
Ronaldo hakumaliza Mechi hii baada ya kuumia na kutolewa nje katika Dakika ya 80.
Timu hizi zitarudiana huko Signal Iduna Park, Jijini Dortmund, Germany Jumanne Aprili 8.

CHELSEA YAPIGWA 3-1 NA PSG! 
Javier Pastore
Paris Saint-Germain, wakicheza Uwanja wa kwao Parc des Princes huko Paris, France, Usiku wa jana waliishinda Chelsea Bao 3-1 katika Mechi ya Kwanza ya Robo Fainali ya UEFA CHAMPIONZ LIGI.

Ezequiel Lavezzi alitangulia kuwapa PSG Bao la kuongoza katika Dakika ya 4 baada kuweka gambani Mpira uliookolewa kwa Kichwa na John Terry na kufumua Shuti moja kwa moja na kumpita Kipa Petr Cech.

Chelsea walisawazisha kwa Penati ya Dakika ya 27 iliyopigwa na Eden Hazard na ilitolewa na Refa Milorad Mazic kutoka Serbia alipoamua Sentahafu wa PSG Thiago Silva ‘kamwangusha’ Oscar.

Hadi Mapumziko Bao zilikuwa 1-1.

PSG walifunga Bao lao la 2 baada ya Ezequiel Lavezzi kupiga Frikiki safi ambayo Kipa Petr Cech alishindwa kuzuia na kumparaza Zlatan Ibrahimovic kisha Mchezaji wa Chelsea David Luiz kuusindikiza wavuni.

Nchezaji alietoka Benchi, Javier Pastore, aliipa PSG Bao la 3 katika Dakika ya 90 baada ya kupokea Mpira wa kurushwa na kuwatoka Cesar Azpilicueta, Frank Lampard na John Terry kisha kupiga Shuti la chini chini na kumshinda Kipa Petr Cech.
Timu hizi zitarudiana huko Stamford Bridge Jumanne Aprili 8.

No comments:

Post a Comment